• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MIFUNGO NA UVUVI

TAARIFA YA IDARA YA MIFUGO NA UVUVI.

Utangulizi.

Idara ya mifugo na uvuvi ni idara inayoshughulikia maendeleo ya mifugo na uvuvi katika ngazi ya wilaya. Ili kuwezesha usimamizi wa sera mbalimbali na sheria zinazohusu mifugo na uvuvi.

Taarifa za watumishi.

Idara ya mifugo na uvuvi ina jumla ya watumishi 22 kati ya hao 6 wapo ofisi kuu na 16 wapo ngazi ya kata na vijiji.

Vitengo vilivyopo.

Idara ya mifugo na uvuvi ina vitengo nane kama ifuatavyo.

  • Wanyama wadogo
  • Afya ya wanyama.
  • Nyama na ngozi.
  • Huduma za ugani
  • Mifumo ya uchungaji.
  • Utambuzi na usajili wa mifugo.
  • Shughuli za maziwa.
  • Uvuvi.

Kazi za kila kitengo.

Wanyama wadogo

      i) Kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika uzalishaji wa  wanyama wadogo na masoko;

(ii) Kuratibu maendeleo yote ya wanyama wadogo kulingana na sera ya taifa.

(iii) kuandaa mipango ya kuimarisha na kundeleza vizazi vya kigeni na asili kwa wanyama wadogo mfano mbuzi kondoo katika wilaya.

(iv)  kupitia mara kwa mifumo ya masoko ya wanyama wadogo ndani ya wilaya.

(v) Kuandaa kila mwezi, robo mwaka, katikati ya mwaka na kila mwaka taarifa juu uzalishaji wa wanyama wadogo  katika wilaya.

               

Afya ya wanyama.

i) kuratibu na  kudhibiti magonjwa ya wanyama na kutokomeza  magonjwa katika wilaya;

(ii) Kusimamia afya ya umma na  mifugo pamoja na  huduma za afya ya wanyama katika wilaya;

(iii) kusimamia  na kudhibiti kuingia na kutoka  kwa wanyama na bidhaa za wanyama katika wilaya;

(iv) Kusimamia ugavi na usambazaji wa pembejeo za mifugo katika wilaya;

(v) Kuandaa programu za muda mfupi na muda mrefu katika kudhiti magonjwa  ya wanyama na kutolkomeza kabisa.

(vi) Kukusanya, kuchambua, kuhifadhi, kusambaza  data za  magonjwa ya mifugo na taarifa nyingine;

(vii) Ufuatiliaji wa magonjwa ya wanyama  na utambuzi wa magonjwa.


Nyama na ngozi.

(i) Kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika biashara ya nyama na  ngozi;

(ii) kuweka madaraja ya wanyama na nyama malengo ya soko na usafirishaji;

(iii) Kuandaa kila mwezi, robo mwaka, katikati ya mwaka na kila mwaka taarifa juu ya uzalishaji wa nyama na masoko;

(iv) Kutekeleza sheria ya nyama katika wilaya;

(v) Ufuatiliaji uzalishaji, ukusanyaji, uhifadhi na masoko ya ubora wa nyama na ngozi;

(vi) Kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya matumizi ya ngozi katika maeneo ya vijijini;

(vii) Kukuza thamani pamoja na ngozi  katika maeneo ya vijijini;


Huduma za ugani.

i) Kuimarisha  kiungo kati ya utafiti-ugani-wakulima na mpango thabiti wa mikutano, majaribio mbalimbali na vitalu vya wanyama makongamano mbalimbali na wafanyakazi wa ugani ngazi ya kata na vijiji pamoja na  wakulima na vikundi.

(ii) kupanga na kushiriki katika uhamasishaji, mafunzo ya wafanyakazi wa ugani katika wilaya na viwango vya walio mstari wa mbele; kupanga, kuongoza na kutathmini mafunzo ya mara kwa mara, kwa wafugaji na shughuli za ugani kwa ujumla.

(iii) Kutengeneza mahusiano imara baina ya watumishi waliopo ngazi ya kata na vijiji pia vikundi kwa ajili ya kuwaongoza katika maendeleo na kutengeneza uhusiano sawa na sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali, na watoa huduma za kilimo na mifugo.

(iv) Kama sehemu ya DFT, kuratibu, kuendeleza na kuongoza mipango ya utoaji huduma za ugani wa mifugo na utekelezaji katika wilaya;

(v) Kusaidia DLFDO katika uundaji wa utumishi wa umma ugani huduma za utoaji mbinu mpya, ufuatiliaji, kuendeleza na kuongoza utekelezaji katika ngazi ya vijiji kata na kutathmini utendaji wa ugani katika wilaya na kuandaa  programu kwa kushirikiana na wilaya ili kuendeleza huduma za ugani katika wilaya.kupanga.

(vi) Kusimamia na kuongoza ukusanyaji wa takwimu zinazohusu huduma muhimu za ugani katika wilaya.

(vii) kuhamasisha, wafanyakazi waliokuwa mstari wa mbele elekezi na kusaidia hujaribu sana kufanya kazi na wafugaji na wakulima makundi mbalimbali kwa ajili ya elimu ya ugani.


Mifumo ya uchungaji.

i) Kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika biashara ya ufugaji;

(ii) Kuratibu masuala yote ya mazingira kuhusiana na mifumo ya uzalishaji wa mifugo;

(iii) Kutathmini na ufuatiliaji wa malisho ardhi, mipaka, matumizi na maendeleo katika wilaya;



Utambuzi na usajili wa mifugo.

(i) Kufanya kazi na watafiti wa mifugo kwa kuboresha aina ya mifugo ya wilaya;

(ii)Kuungana  kwa kushirikiana na taasisi nyingine za kuanzisha uboreshaji wa mifugo ya wilaya;

(iii)  Kusajili na kusimamia secta zote binafsi zinazojihusisha na afya za wanyama katika wilaya.

(iv) Kuandaa  na kuratibu utafiti wa idadi ya mifugo na sensa;


Shughuli za maziwa.

(i) Kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika ufugaji ng'ombe wa maziwa na usindikaji.

(ii) Kuratibu shughuli zote zinazohusu uzalishaji wa ng’ombe wa maziwa katika wilaya kulingana na sera ya taifa.

      (iii)Kuandaa mipango na kuendeleza njia ya kuimarisha ng’ombe wa maziwa wa  kigeni na ng’ombe wa asili.

      (iv) Mapitio ya mara kwa ya uzalishaji wa maziwa na bidhaa za maziwa na kuandaa mifumo ya masoko.


Uvuvi.

(i) Kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika uvuvi ufugaji na usindikaji;

(ii) Kuratibu samaki wote wa wilaya kuzaliana  kwa mujibu wa sera ya taifa;

(iii) Kuandaa  na kuendeleza njia ya kuimarisha sekta ya uvuvi;

(iv) Kupitia mara kwa mara mifumo ya masoko ya samaki na bidhaa zao katika Wilaya.

(v) Kutekeleza sheria ya uvuvi katika ngazi ya wilaya;

(vi) Kuandaa kila mwezi, robo mwaka, katikati ya mwaka na kila mwaka taarifa juu ya utendaji wa uvuvi katika wilaya


Kazi zinazofanywa na idara kwa ujumla.

Idara ya mifugo na uvuvi inashughulikia maendeleo yote yahusiyo mifugo na samaki pamoja na kuunganisha utafiti na wafugaji.  Pia kuratibu kuingia na kutoka kwa mifugo semu moja na nyingine ndani ya wilaya na nje ya wilaya.

Kuandaa mazingira mazuri ya uwekezaji ndani ya wilaya katika mifugo na samaki. Kutoa elimu bora kwa wafugaji juu ya ufugaji bora na wenye tija.

Utaratibu wa kupata huduma mbalimbali.

Idara ya mifugo na uvuvi inatoa huduma mbalimbali katika wilaya.

  • Vibali vya kusafirishia mifugo. Ili kupata huduma hii ni lazima kumuona afisa mifugo aliyopo katika eneo husika na akupe barua ya kuja nayo ofisi kuu ili kupata kibali cha kusafirishia.
  • Kutoa elimu ya mifugo na uvuvi kwa mtu mmoja moja na vikundi. Ili kupata huduma hii ni kumuona muhusika wa mifugio na uvuvi katika eneo husika.
  • Kutoa ushauri wa masuala mbalimbali yahusiyo mifugo. Pia ili kupata huduma inatakiwa kuonana na muhusika wa mifugo ndani ya wilaya.
  • Kusimamia afya mifugo katika wilaya. Ili kupata huduma hii ni kumuona afisa mifugo na uvuvi katika eneo husika.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 WILAYA YA WANGING'OMBE December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI March 18, 2019
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA July 09, 2019
  • MWENGE WA UHURU September 13, 2019
  • Itizame yote

Habari mpya

  • Utekelaji Anwani za Makazi wafikia asilimia 67 kwa Ikoa yote

    March 31, 2022
  • VIJANA 246 WAPATIWA MAFUNZO ANWANI ZA MAKAZI

    March 22, 2022
  • WANANCHI KATA YA IMALINYI WAJENGEWA KITUO CHA AFYA

    March 17, 2022
  • WANANCHI KATA YA WANGAMA WAJENGEWA KITUO CHA AFYA

    March 12, 2022
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • REGISTRATION OF ALLIED HEALTH PROFESSIONALS
  • Mfumo wa maombi ya Ajira

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • Halmashauri ya Mji Makambako
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.