• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

Kilimo

                                    

 

 UTANGULIZI

Idara ya kilimo, Umwagiliaji na Ushirika ni mojawapo ya Idara muhimu sana katika mamlaka ya serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe.

Idara ina majukumu makubwa ya kusimamia na kufuatilia shughuli zote zihusuzo kilimo cha mazao ya aina zote yaani chakula na biashara, kusimamia masuala yote ya umwagiliaji na mambo ya ushirika katika eneo lote la Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe.

Idara ina vitengo vitatu tu yaani Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika.

 

MAJUKUMU YA IDARA

Kumshauri Mkurugenzi Mtendaji masuala yote yanayohusu Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

Kutoa miongozo, sera na kanuni za kilimo bora cha mazao ya aina zote

Kuratibu shughuli zote zinazohusiana na uendelezaji mazao

Kushauri na kusimamia shughuli zote za umwagiliaji kwa kushirikiana na wataalam kutoka tume ya umwagiliaji kanda na Taifa

Kuandaa taarifa za utekelezaji wa malengo yaliyopangwa na zinginezo na kuziwasilisha sehemu husika

Kutoa ushauri wa kitaalam juu ya uzalishaji wa mazao ya aina zote yanayostawi na yanayoweza kustawi katika Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe

Kuandaa, kuratibu na kupanga mipango ya maendeleo na bajeti ya idara ya kila mwaka, taarifa za utekelezaji na kuziwasilisha taarifa kama inavyotakiwa.

Kushirikiana na taasisi za utafiti na wadau wengine kufanya majaribio ya tekinolojia mbalimbali za kilimo.

Kuratibu watoa huduma wote wa sekta ya kilimo, umwagiliaji na ushirika

Kuhamasisha, kuunda na kusimamia uendeshaji wa vyama vya ushirika na vikundi vingine.

TAARIFA ZA UTEKELEZAJI

Taarifa za mwezi, robo mwaka, nusu mwaka na mwaka zinaandaliwa za mpango wa maendeleo ya kilimo za kijiji, kata na Halmashauri.

Taarifa zote za utekelezaji za watumishi wa idara wa Halmashauri na wadau wa sekta ya kilimo, umwagiliaji na ushirika zinaandaliwa na kuwasilishwa kwenye kamati za viongozi ndani ya Wilaya, mkoa na Taifa.

Taarifa za ufuatiliaji na tathimini zinaandaliwa. Miradi, Mvua, watumishi nk.

MASWALI MBALIMBALI YANAYOULIZWA NA WANANCHI

Ruzuku ya pembejeo zingine za mazao kama ilivyo kwa mbolea na mbegu za mahindi

Kuibuka kwa magonjwa yenye tabia mpya na sugu kutibika

Kuibuka tabia mpya za wadudu katika kushambulia mimea na usugu wao dhidi ya madawa

Bei kubwa ya pembejeo. Kwa sasa serikali imetoa bei elekezi ya DAP na UREA.

 

HATUA MBALIMBALI WANAZOTAKIWA KUFUATA KATIKA KUPATA HUDUMA

Kuwatumia (kwa karibu) wataalam wa ugani kilimo katika hatua zote za uzalishaji

Matumizi sahihi ya viuatilifu kwa kufuata vipimo sahihi, kiuatilifu sahihi, muda sahihi na kuvaa vifaa kinga

Wataalam kupata mafunzo mara kwa mara ili kuendana na wakati

Kutumia vema kanuni za kilimo bora

TAARIFA ZA MILIPUKO YA WADUDU NA MAGONJWA KUCHUKUA WANANCHI

Wadudu

Magonjwa

 

  1. USHIRIKA
    1. SERA YA MAENDELEO YA USHIRIKA:

Sera inatambua misingi ya ushirika ya kimataifa ambayo ni;

Uanachama wa hiari

Demokrasia

Kujitegemea kiuchumi

Uhuru wa maamuzi

Elimu na mafunzo

Ushirikiano

Kujali Jamii.

 


    1. DIRA YA SERA YA USHIRIKA TANZANIA NI:

“KUUNDA VYAMA VYA USHIRIKA IMARA NA ENDELEVU VYENYE UWEZO WA KUKIDHI MAHITAJI YA WANACHAMA YA KIUCHUMI NA KIJAMII”

 

Jukumu  kuu la sera ni kuandikisha na kuendeleza vyama vya ushirika ambavyo ni:-

Msingi wake ni wanachama

Vinafanya shughuli zake kiushindani vikiwa vyombo huru vya kiuchumi

Vinawajali wanachama kwa ujumla wao

Vinafanya kazi kwa manufaa ya maendeleo ya kiuchumi na kiuchumi ya wanachama wenyewe na Jamii.


    1. SHERIA YA VYAMA VYA USHIRIKA:

Inawapa wanachama uwezo na mwongozo wa kuweka mfumo unaokidhi mahitaji yao

Inatambua umuhimu wa kuwa na vyama vya Ushirika vya msingi na shirikisho

Inatambua kuwepo kwa vyama vya Ushirika vya kati na kilele kutegemeana na matakwa na maamuzi ya wanachama

Inaweka utaratibu wa uchaguzi wa viongozi na ajira kwa watendaji unaozingatia maadili ya uongozi

Inaelekeza uandikishaji wa vikundi vya kiuchumi vya wananchi kabla havijawa vyama vya Ushirika kamili

Inahimiza ukaguzi wa hesabu za vyama na utoaji taarifa

Kanuni za vyama vya Ushirika zinaelekeza jinsi utekelezaji wa sheria hiyo ya Ushirika kulingana na mchepuo.


    1. KAZI ZA IDARA YA USHIRIKA:

Kuwezesha uandikishaji wa vikundi vya kiuchumi kuwa vyama vya Ushirika, kushauri kufuata na kusimamia  vyama vya Ushirika.

Kusimamia utekelezaji wa sheria ya vyama vya Ushirika

Kufanya uchunguzi na ukaguzi kuhusu uendeshaji wa shughuli za Ushirika

Kujasirisha wanachama na viongozi kwa kuwawezesha kupata elimu na stadi za kuendeleza vyama vyao

Kutoa huduma za ushauri na kuweka mazingira muafaka yatakayowezesha ukuaji na uendelezaji wa Ushirika

Kuhakikisha kuwa kesi zinazohusisha vyama vya Ushirika zinashughulikiwa kwa haki.

 


    1. MWONGOZO WA UANZISHAJI WA VYAMA VYA USHIRIKA VYA KILIMO NA MASOKO ( AMCOS )

 

USHIRIKA:

Ni muungano wa watu waliokubali kuendesha shughuli zao za Kiuchumi kwa pamoja na kuinua shughuli zao za maisha.

CHAMA CHA USHIRIKA:

Kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika Na 20 ya Mwaka 2003,

Ni muungano wa watu ambao kwa hiari wameamua kujiunga kwa pamoja kuunda chombo kinachoongozwa kidemokrasia ambao huchangia kiasi kinachohitajika kufanya mtaji unaohitajika kuunda chombo hicho wanaokubali kupokea manufaa na  hasara yatokanayo na shughuli za chombo hicho.

AINA:

Zipo aina nyingi kutegemeana na mahitaji mfano, SACCOS, AMCOS n.k.  Idadi ya wanachama hutegemea shughuli ya kiuchumi ambayo umoja huo unaundwa.  Kwa vyama vya Ushirika kilimo na Masoko idadi inayohitajika ili chama kisajiliwe ni watu kuanzia angalau hamsini (50).

Chama cha Ushirika ni kwa manufaa ya wanaushirika.  Wadau wengine wanaweza kupata manufaa kutokana na shughuli za ushirika , kama vile kupata bidhaa ambazo zinatokana na shughuli za chama.

SHUGHULI:

Chama cha Ushirika cha  Kilimo na Masoko  dhumuni / lengo lake kuu ni kutoa huduma ya pembejeo za kilimo, kununua,kutafuta Masoko , kusindika, kusambaza na kuuza mazao ya kilimo.

UENDESHAJI:

Vyama vya Ushirika huendeshwa kwa mujibu wa masharti ya chama chenyewe, kanuni za mwaka 2004 na sheria Na. 20 ya mwaka 2003 ya vyama vya Ushirika.  Ushirika huendeshwa na wanachama ambao wameuunda.  Wanachama wa chama cha Ushirika ni watu wenye umri usiopungua miaka 18 wenye akili timamu wanaojishughulisha na shughuli zinazowaunganisha.


    1. UTARATIBU WA UANZISHAJI WA USHIRIKA:

HATUA ZAKE:

Kuwe na watu ambao wako tayari kuanzisha Ushirika wa aina yoyote ile.  Kwa hiari yao mfano:

Ushirika wa Kilimo na Masoko – AMCOS = wanachama 50

Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) = wanachama 20

Ushirika wa taaluma mfano: Seremala, Ufundi washi, Umeme, Ufundi magari n.k. wanachama 20

Bustani n.k. wanachama 10.

             

Kuwepo kwa mkutano mkuu wa Uhamasishaji wa Ushirika

Afisa Ushirika Mtoa Elimu ya Ushirika  Viongozi na wadau wengine Wahamasishaji.

Kuwepo kwa mkutano mkuu wa uanzilishi wa Ushirika:

Afisa Ushirika atakuwa mwenyekiti wa muda

Watachaguliwa viongozi wa muda (Formalization Committee)

Watapendekeza viwango vya kuchangia ilikuwa Mwanachama  ikiwa ni pamoja na;

.  Kiingilio - kitakachopendekezwa

.  Hisa 5 @ Tshs.

.  Akiba ya mwezi/mwaka Tshs.

Mapendekezo ya kuandaa Katiba/Masharti ya chama

Kuwepo kwa eneo la ofisi ya chama

Pendekezo la kufungua akaunti Benki na kuteua watia saini

Uongozi wa muda kusaidiana na Afisa Ushirika kwenye

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE 31 JULAI 2024 July 31, 2024
  • KUITWA KWENYE USAIL September 27, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA UMILIKISHWAJI ARDHI February 13, 2021
  • Itizame yote

Habari mpya

  • TUZO ZATOLEWA KWA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025, NGAZI YA WILAYA - WANGING'OMBE.

    May 16, 2025
  • VIJIJI 10 VYA WANGING'OMBE KUNUFAIKA NA HATI ZA KIMILA 3,010

    May 13, 2025
  • BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI ROBO YA PILI YA MWAKA 2024/2025

    January 29, 2025
  • HERI YA SIKU YA KUZALIWA, MKURUGENZI MTENDAJI, DKT. PETER MAIGA NYANJA

    January 28, 2025
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.