• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

Utalii

HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING’OMBE

IDARA YA ARDHI NA MALIASILI

VIJUE VIVUTIO VYA UTALII KATIKA WILAYA YA WANGING’OMBE

Wilaya ya Wanging’ombe imebahatika kuwa na vivutio vingi vya utalii ambavyo vinaweza kuchangia

mapato makubwa kutokana na wageni mbalimbali wanaoweza kutembelea vituo kwa ajili ya kujionea

maajabu mbalimbali katika vivutio hivyo. Vivutio vinavyopatikana katika wilaya ya Njombe ni pamoja

na Mapango na Msitu wa hifadhi wa Nyumbanitu, mwamba wenye ramani ya bara la Afrika, pori la

akiba la Mpanga Kipengere, Eneo la ardhi oevu la Lihogosa, Kilele cha mlima wa Fulanyingi, eneo la

kihistoria la Mdandu, Mapango na Msitu wa Mayiviyivi na Kanisa la kilutheri la Kidugala.

A. MAPANGO NA MSITU WA NYUMBANITU

Mapango na Msitu wa Nyumbanitu viko katika kijiji cha Mlevela, kata ya Igima tarafa ya Mdandu.

Msitu huu ni wa maajabu sana kwani miti yake na mimea yake iko pale kwa karne nyingi.

Inaaminika kuwa makabila mengi ya mikoa ya Iringa, Mbeya, Morogoro na Ruvuma yana

asili ya eneo la Nyumbanitu na kuwa wahenga wa wabena walizikwa katika eneo hili.

Sifa za Pekee za Msitu na Mapango

a. Uwepo wa eneo la Tambiko.

b. Kuwepo kwa kuku weusi ndani ya msitu wasiofugwa.

c. mapango makubwa ambayo watu zaidi ya mia moja

wanaweza kuishi kwenye mapango. Mapango hayo

yalikuwa yanatumika sana wakati wa vita.

d. Aina (Sp) pekee za miti.

Aina ya Utalii unaofaa

a. Utalii wa kiutamaduni.

b. Utalii wa kupiga picha.

c. Utalii wa kutembelea na

kupumzika kwenye mapango.

Msitu wa Nyumbanitu Msitu wa Nyumbanitu Mapango ya Nyumbanitu

S. L. P 624

NJOMBE

2

B. MWAMBA WENYE RAMANI YA BARA LA AFRIKA

Mwamba wenye ramani ya bara la Afrika uko katika kijiji cha Igodivaha, kata ya Kidugala, tarafa ya

Imalinyi. Eneo hili lina uzuri wa kipekee kimandhari na pia utashangazwa na mwamba wenye ukubwa

unaokadiriwa kuwa ekari 14 na sehemu ya mwamba huu ina sura mithili ya ramani ya bara la Afrika.

Mwamba/jiwe hili limezungukwa na msitu wa hifadhi wa Lwivala wenye miti aina ya miombo

inayofanya eneo hili kuwa tulivu na lenye mandhari nzuri.

C. PORI LA AKIBA LA WANYAMAPORI LA MPANGA/KIPENGERE

Pori hili linapatikana katika wilaya za Wanging’ombe, Makete na Mbarali. Pori hili linasimamiwa na

shirika la taifa la hifadhi ya wanyama pori (TANAPA). Pori hili lina sifa ya kuwa na mimea na

wanyama wa aina mbalimbali (baadhi wakiwa adimu). Inaaminika kuwa kuna zaidi ya aina 28 za

wanyama pori; baadhi ya wanyama hao ni nguruwe pori, ngiri, nyani, fisi, mbega wekundu,

kakakuona, na mbweha wenye mgongo mweusi. Pia wapo mamba, nyoka na ndege wa aina

mbalimbali. Katika pori hili pia kuna mandhari nzuri ya hali ya miinuko na mabonde na maporomoko

na vyanzo vya maji.

Aina ya utalii inayofaa kufanywa eneo hili ni kupiga picha, kupanda milima n.k.

Mwamba wenye ramani ya barara la Afrika

Sifa kwa shughuli za Utalii

a. Mwamba wenye ramani ya Asili.

b. Sehemu ya kufanyia Tafrija.

Aina ya Utalii Unaofaa

a. Utalii wa mazingira.

b. Utalii wa picha pamoja na

c. sehemu za kupumuzika.

Baadhi ya Maeneo ya pori la Mpanga Kipengere

3

D. ENEO OEVU LA LIHOGOSA

Eneo hili oevu la Lihogosa liko kando kando ya barabara kuu inayotoka Njombe kuelekea Makambako

na liko katika vijiji vya Igima na Mhaji.

Eneo oevu la Lihogosa limebainika kutembelewa na ndege maji wa aina mbalimbali, lina samaki, na

lina uzuri wa kipekee wa mandhari na maeneo mazuri ya tafrija. Bonde la Lihogosa lina nyasi fupi za

kijani na maji yaliyotuama.

Eneo oevu la Lihogosa linafaa kwa utalii wa uvuvi, utalii wa kuzunguka bwawa kwa kutumia

mitumbwi, kuogelea, kuona ndege, utalii wa picha na tafrija/mapumziko. Eneo hili linafaa pia kwa

uwekezaji wa lodge na campsite.

E. MLIMA FULANYINGI

Kilele cha mlima Fulanyingi kinapatikana katika kijiji cha Imalilo kata ya Wangama. Eneo hili ndio

uwanda wa juu kabisa kuliko maeneo yote ya wilaya ya Wanging’ombe na Njombe, hivyo kilele hiki

hutoa fursa ya kuona mandhari pana ya wilaya ya Wanging’ombe na maeneo mengine jirani. Pia

katika mlima Fulanyingi kuna vyanzo vingi vya maji zaidi ya 98.

Eneo hili linafaa sana kwa utalii wa kupanda milima, Kujionea wanyama na mandhari nzuri ya

maumbile ya kijiografia, sehemu za mapumziko na utalii wa picha.

Eneo la kilele hiki linafaa kwa uwekezaji wa miundombinu ya kupumzikia (campsite).

F. MAENEO YA KIHISTORIA YA MDANDU

Maeneo ya kihistoria ya Mdandu yako katika kijiji na kata ya Mdandu, tarafa ya Imalinyi. Maeneo ya

kihistoria ya Mdandu yanajumuisha Mahakama na Boma la Wajerumani, njia ya watumwa wa kabila

la Wabena, Wakinga na Wapangwa pamoja na mti aina ya Mdzombe ambao ni asili ya jina la Mkoa wa

Njombe kwa sasa.

Eneo la Mdandu lina umuhimu mkubwa kwa historia ya Mkoa wa Njombe. Hii inatokana na eneo hilo

kuwa na sifa zifuatazo:-

a. Makazi na ofisi za kwanza za utawala wa Kijerumani (German Boma). Wajerumani walichagua

Mdandu kuwa makao makuu ya wilaya ya Njombe (Mkoa wa Njombe kwa sasa). Baada ya

Wajerumani kupigwa na Waingereza katika vita kuu ya kwanza ya dunia, Waingereza

waliamua kuhamisha makao makuu ya Wilaya kuwa Njombe. Hivyo waliamua kuhamisha

’boma’ hiyo kuja mahali ilipo Njombe kwa sasa. Mahakama iliyokuwa ikitumiwa na

Wajerumani ipo hadi sasa ila haitumiki kutokana na ubovu wa jengo.

Eneo oevu la Lihogosa

4

b. Soko la Mdandu. Soko hilo lipo na halitumiki kwa madhumuni ya soko.

c. Barabara ya watumwa. Wakati biashara ya utumwa ikifanyika, watu wa Ubena, Ukinga na

Upangwa walikusanywa kutoka maeneo hayo kwenda pwani kwa ajili ya kuuzwa. Chifu wa

wabena aliyeitwa Mbeyela alishiriki biashara ya watumwa kwa kutoa ushirikiano kwa Waarabu

kwa kuwa alikuwa akipata silaha na vitu vingine kutoka kwa Waarabu.

d. Makazi ya Chifu wa Ubena. Makazi ya Chifu yapo katika eneo la Mdandu.

e. Mti wa Mdzombe. Katika eneo hili kuna mti ambao jina lake ndilo asili ya jina la Mkoa wa

Njombe. Hii inatokana na Wajerumani kushindwa kutamka jina hilo inavyostahili hivyo

kutohoa jina hilo na kuita Njombe.

Utalii unaofaa katika maeneo haya ya kihistoria ni ule wa kujifunza historia ya Wabena.

G. KANISA LA KILUTHERI LA KIDUGALA

Kanisa la Kilutheri la Kidugala liko katika kijiji na kata ya Kidugala, tarafa ya Imalinyi. Kanisa hili ni la

kihistoria na kivutio cha utalii kwa sababu zifuatazo:-

a. Kuwa na jengo lenye umri wa zaidi ya miaka 100. Kanisa la Kidugala lilikamilika kujengwa

mnamo mwaka 1898.

b. Kuwepo kwa nyaraka za kale zenye masimulizi kuhusu historia ya Wabena kama walivyokutwa

na Wajerumani na ushiriki wao katika vita ya Maji maji.

H. MSITU WA ASILI WA MAYIVIYIVI NA MAPANGO

Msitu na mapango ya Mayiviyivi yako katika kijiji cha Igagala, kata ya Ulembwe, tarafa ya Imalinyi.

Katika msitu huu kuna mapango yenye vyumba mbalimbali. Eneo la msitu na mpango ya Mayiviyivi

hutumika kwa shughuli za matambiko na ni eneo linalofaa kwa utalii wa kiutamaduni.

Kanisa la Kilutheri la Kidugala

5

CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI SEKTA YA UTALII

a. Ukosefu wa kwa ajili ya kutekeleza shughuli za sekta ya Utalii katika wilaya, hivyo sekta hii

inategemea fedha za makusanyo ya halmashauri.

b. Kukosekana kwa huduma ya tovoti ili kurahisisha utangazaji wa vivutio ili kuweza kupata

wageni kwa urahisi zaidi.

c. Ukosefu wa wataalamu wenye fani ya Utalii katika halmashauri ya Wanging’ombe.

d. Kukosekana kwa tafiti za kina na mara kwa mara ili kupata taarifa sahihi za vivutio.

e. Kukosekana kama hotel, maeneo ya kupumzika, huduma za vyoo nk karibu na vivutio.

FURSA ZILIZOPO KATIKA MAENEO YA VIVUTIO

a. Uwezekano wa kutengeneza sehemu za huduma za kitalii kama vile maeneo ya kupumzikia

watalii, vyoo, sehemu za chakula, malazi na zile za kutupia taka.

b. Uwezekano wa kuvitangaza vivutio kitaifa na kimataifa ili kuvutia watalii wengi zaidi

kulitembelea.

MIKAKATI YA UBORESHAJI VIVUTIO VYA UTALII

a. Kushirikisha wanajamii wanaoishi katika maeneo ya vijiji vinakopatikana vivutio tajwa

kutengeneza miundombinu ya vyoo, sehemu za kupumzikia watalii, kutupia taka, kwa

kutumia raslimali zinazopatikana katika maeneo ya vijiji vyao.

b. Kuzijengea uwezo kamati za Maliasili za vijiji juu ya umuhimu wa utunzaji wa Mazingira

ya vivutio vya utalii na utunzaji wa kumbukumbu mbalimbali za utalii.

c. Kuyabainisha maeneo mbalimbali ya uwekezaji wa miundombinu ya utalii zikiwemo

hoteli za kitalii na kuwakaribisha wadau kuwekeza katika maeneo jirani na vivutio

ikiwemo maeneo ya Igodivaha – (Kata ya Imalinyi), Mlevela/Nyumbanitu- (Kata ya

Mdandu).

d. Kuandaa utaratibu wa kuvitangaza vivutio vyote vilivyopo ndani ya wilaya.

e. Kuanza mchakato wa kuandika andiko la Mapendekezo (Proposal) ya uboreshaji wa

miundombinu ya vivutio vya utalii itakayosambazwa kwa wadau mbalimbali ili

kuhamasisha uwekezaji na Uchangiaji wa uboreshaji wa miundombinu itakayobainishwa.

--------------------------

Kasmiri David

Forest Officer I - H/W

WANGING’OMBE

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 WILAYA YA WANGING'OMBE December 14, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI March 18, 2019
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA July 09, 2019
  • MWENGE WA UHURU September 13, 2019
  • Itizame yote

Habari mpya

  • Utekelaji Anwani za Makazi wafikia asilimia 67 kwa Ikoa yote

    March 31, 2022
  • VIJANA 246 WAPATIWA MAFUNZO ANWANI ZA MAKAZI

    March 22, 2022
  • WANANCHI KATA YA IMALINYI WAJENGEWA KITUO CHA AFYA

    March 17, 2022
  • WANANCHI KATA YA WANGAMA WAJENGEWA KITUO CHA AFYA

    March 12, 2022
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • REGISTRATION OF ALLIED HEALTH PROFESSIONALS
  • Mfumo wa maombi ya Ajira

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • Halmashauri ya Mji Makambako
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.