• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

Idara ya Maendeleo ya Jamii


SHUGHULI ZINAZOFANYWA NA IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

Idara ya Maendeleo ya Jamii ni miongoni mwa Idara inayotoa huduma ya ugani katika jamii kwa kutumia njia shirikishi katika kubuni,kupanga,kutekeleza na kufuatilia miradi ya maendeleo ya jamii husika katika Wilaya ya Wanging’ombe.

Kadhalika idara inajihusisha na uhamasishaji wananchi juu ya:

i.Umuhimu wa kuchangia nguvu kazi na fedha ya miradi ya kujitegemea

ii. Kuwezesha usajili wa vikundi vya kijamii

iii. Kuwezesha kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa kwa vikundi vya vijana na wanawake.

iv. Kuwezesha tafiti za kijamii

v. Kuhamasisha jamii juu ya  usawa wa kijinsia  na kuondokana na mila na desturi zinazokwamisha maendeleo

vi. Kuelimisha jamii juu ya kuziua ukatili wa kijinsia,ukeketaji wasichana na wanawake,Ukweli kuhusu UKIMWI na  kuondokana na dhana potofu za ushirikina na uchawi.

vii. Kusimamia Miradi ya  ikiwemo Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF III) na wa Mapambano dhidi ya UKIMWI.

viii.Kuwezesha uhamasishaji na usajili wa Jumuiya za Watumia maji

1.0 KUSIMAMIA MIFUKO YA MAENDELEO YA WANAWAKE NA VIJANA.

Idara ya maendeleo ya Jamii inawezesha vikundi vya wanawake na vijana kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF) na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana (YDF).

1.1 MFUKO WA MAENDELEO YA WANAWAKE 

Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake ulianzishwa Mwaka 1993 kwa azimio la Bunge “Exechequer and Audit Ordinance ya Mwaka 1961.

Mfuko huu unachangiwa 5% ya mapato ya Halmashauri na Serikali Kuu yaani Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii.

1.1.1 Lengo la Mfuko:

  • Kutoa mikopo kwa Wanawake ili kuwaimarisha kiuchumi.
  •  Kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa Wanawake
  • Kuwa kama Mfuko wa dhamana
  • Kuongeza ajira na kipato kwa wanawake katika sekta isiyo rasmi
  • Kuwajengea wanawake tabia ya kujiwekea akiba
  • Kutafuta vyanzo vya fedha  

 Walengwa wa mfuko huu ni wanawake wote wa Tanzania wenye Umri wa miaka 15 na kuendelea wenye uwezo wa kufanya kazi za uzalishaji mali.

1.1.2 SIFA ZA VIKUNDI VYA WANAWAKE 

i.Kikundi cha wanawake watano(5)

ii.Kikundi kiwe kimesajiliwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii(Halmashauri ya Wilaya/Mji)

iii. Kikundi kiwe na mradi wa kiuchumi

iii.Kikundi kimewasilisha maombi ya mkopo kupitia kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji na Kata

iv.Kikundi kijadiliwe na kupitishwa na  Kata (Kamati ya mikopo ya ngazi Kata).

v. Kamati ya mikopo ngazi ya Halmashauri itapitia na kuidhinishwa.

1.2.1 Uwezeshaji mikopo kwa Vikundi vya wanawake kiuchumi:

  • Mwaka
  • Bajeti
  • Kiasi cha Mikopo
  • Halmashauri
  • vikundi
  • Serikali Kuu
  • Vikundi

2013/14

38,624,363

4,500,000

9

0

0

2014/15

40,146,300

10,000,000

12

0

0

2015/16

40,822,340

23,000,000

21

7,000,000

6

2016/17

40,500,000

44,500,000

35

0

0

JUMLA

160,093,003
82,000,000
77

7,000,000

6

 

Katika kipindi cha Mwaka 2013/14 hadi 2017 jumla ya vikundi 83 vya Wanawake  vimewezeshwa Jumla ya Tsh 82,000,000 kutokana na mchango wa mapato ya ndani  Halmashauri na toka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto.

 

 

1.2.0 Mfuko wa Maendeleo ya Vijana

1.2.1 Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ulianzishwa Mwaka 1993/94 chini ya kifungu cha Na.17(i) cha The Exchequer and Audit ordinance (cap.439) Na,21 of 1961”

  • Mikopo toka Serikali Kuu inatolewa kupitia miradi ya vijana itakayoidhinishwa kati ya Halmashauri,Mikoa na Wizara ya Maendeleo ya Vijana na utamaduni.
  • Mikopo toka Halmashauri itatolewa kwa kuidhinishwa na Kamati za Mikopo za Kata na Halmashauri

1.2.2 Walengwa wa mfuko huu ni:

  • Vijana wote (kike/kiume) raia wa Tanzania kuanzia  Umri wa miaka 15 – 35
  • Vijanawenye uwezo wa kufanya kazi za uzalishaji
  • Vikundi vinavyopewa  mikopo kutoka kwenye Mfuko wa Maendeleo ya  vijana ni vile vilivyopitishwa / ilidhinishwa kuanzia ngazi ya kijiji, Kamati ya mikopo ngazi ya Kata na  hatimaye kamati ya mikopo ngazi ya Halmashauri.
  • Mikopo iliyotolewa kwa Vikundi vya Vijana tangu 2013/14 hadi 2016/17

  • Mwaka

    Bajeti

    Kiasi cha Mikopo

    Halmashauri

    vikundi 

    Serikali Kuu

    Vikundi

    2013/14

    38,624,363

    4,500,000

    6

    0

    0

    2014/15

    40,146,300

    10,000,000

    18

    0

    0

    2015/16

    40,822,340

    21,000,000

    7

    0

    0

    2016/17

    40,500,000

    29,500,000

    22

    0

    0

    JUMLA

    160,093,003
    65,000,000
    53

    0

    0

  • 1.2.3 Sifa ya Wakopaji:

    Katika kipindi cha Mwaka 2013/14 hadi 2017 jumla ya vikundi 53 vya Vijana vimewezeshwa Jumla ya Tsh 61,000,000 kutokana na mchango wa mapato ya ndani  Halmashauri.


    • Vijana Wajiunge kwenye vikundi vya watu Watano na wawe na shughuli wanazofanya za kujiongezea Kipato
    • Kikundi kiwe na  vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 35 tu.
    • Kikundi kiwe kimesajiliwa na Halmshauri.
    • Barua ya maombi ya mkopo inatakiwa kupitishwa kuanzia ngazi ya kijiji na kata ikiwa imeambatanishwa na andiko la kazi ya uzalishaji inayotegemewa kufanywa na wakopaji  na hatimaye andiko hilo la mradi linapitiwa na wataalum ngazi ya Halmashauri baada ya mchujo wa maandiko yaliyokidhi vigezo maombi yao ya mikopo hupelekwa katika kamati ya Mikopo ya Wilaya

  • Kikundi vya wanachama watano,na wawe na shughuli wanazozifanya za kujiiongezea kipato

    2.2 SIFA ZA WAKOPAJI

    Mkopaji (Vikundi) wanapaswa kurudisha kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa kwa robo husika katika SACCOs aliyopokelea mikopo.

    Mikopo hii hutozwa riba ya 10% inayolipwa Halmashauri na 2% kwa vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa(SACCOS) na kufanya riba ya 12% katika muda ndani ya  miezi 12 (mwaka mmoja) ambayo imegawanyika kwa robo 4 kila robo.

    Fedha za Mikopo hii hutokana na mchango wa Halmashauri tokana 5% ya mapato yake ya ndani.

    Mikopo ya Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake  hutolewa kupitia  vyama vya ushirika (SACCOS) vilivyo karibu na  Kijiji kinapotoka kikundi husika, hii inasaidia ufuatiliaji wa vikundi na marejesho ya mikopo kwa kuwa fedha hizi ni mfuko maalum (revolving Fund) ni lazima waliokopeshwa warudishe ili vikundi vingine vikopeshwe.

     2.1. UTARATIBU WA UTOAJI MIKOPO(WDF)

    2.0 MFUKO WA MAENDELEO YA WANAWAKE(WDF)

    Uwezeshaji mafunzo ya ujasiriamali kwa Vikundi vya Vijana katika Kijiji cha Katenge Kata ya Wanging’ombe.

    • Kikundi kiwe kimesajiliwa na Halmashauri
    • Kikundi kiwe na  wanawake wenye umri wa kuanzia miaka 15 na kuendelea  na wenye uwezo wa kufanya kazi za uzalishaji.
    • Barua ya maombi ya mkopo inatakiwa kupitishwa kuanzia ngazi ya kijiji na  Kamati ya Mikopo ya ngazi ya Kata ikiwa imeambatanishwa na andiko la kazi ya uzalishaji inayotegemewa kufanywa na wakopaji  na hatimaye andiko hilo la mradi linapitiwa na wataalam ngazi ya Halmashauri baada ya mchujo wa maandiko yaliyokidhi vigezo maombi yao ya mikopo huptishwa katika kamati ya Mikopo ya Wilaya
  • Na.
    JINA LA MRADI
    WALENGWA
    KIJIJI
    KATA
    1
    Ufugaji wa Mbuzi
    i.
    Vikundi 4
    Igando
    Luduga


    ii.
    Vikundi 2
    Sakalenga
    Itulahumba


    iii.
    Vikundi 3
    Mpululu
    Udonja
    2.
    Ujenzi wa nyumba
    iv
    Mwalimu S/M
    Ivigo
    Igosi
    3.
    Ujenzi wa madarasa S/M
    v.
    Wanafunzi S/M
    Msimbazi
    Uhambule

    Katika kipindi cha Mwezi Septemba,2017 Halmashauri imepokea fedha kwa ajili ya Miradi mikuu 3 ya ufugaji mbuzi,ujenzi wa nyumba ya Mwalimu Shule ya Msingi Ivigo na Ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Msimbazi ambayo imetambulishwa na kuingiziwa fedha kiasi cha Jumla Tsh.235,079,737.57 kwa ajili ya utekelezaji kama ifuatavyo:

    3.3. UTAMBUZI WA MIRADI 

     

     

     

    MPANGO WA TASAF III: Kikundi cha (kuweka na kukopa) COMSIP  Kijiji cha Mayale:Agosti,2017

     

     

    TASAF III (OPEC): Mradi wa ufugaji Kuku Bi. Asia Ngole Kijiji cha Mayale: Agosti,2017

     

    Mpango wa TASAF III: Nyumba ya Walimu Shule ya Sekondari Usuka-Kata ya Usuka: Agosti,2017

     

     

    Mpango wa TASAF: Wanakikundi wakikamilisha ujenzi wa kivusha maji cha Mfereji wa umwagiliaji Kijiji cha Mtapa: Agosti,2017

     

     

     

    Bi.Anna Mwinuka mlengwa wa TASAF III(OPEC) anafanya biashara ya mayai ya kuku wa kienyeji na anajenga nyumba ya kisasa Kijiji cha Mayale: Septemba,2017. 

     

     Mpango wa TASAF III(OPEC) Bi.Anna Mwinuka Kijiji cha Mayale akifanya biashara ya mayai ya kuku wa kienyeji.

     

    No
    KATA
    Kijiji
    Jina la Mradi
    Kiasi kilichotengwa
    Hatua za utekelezaji 
    1
    Igwachanya
    Mtapa
    Kivusha maji ya mfereji wa umwagiliaji
    66,389,360.71
    Ujenzi umekamilika. Maandalizi ya vyeti vya kuzindua miradi inaendelea.
    2
    Mdandu
    Itambo
    Ufugaji wa mbuzi na Kuku
    22,321,428.56
    Mradi umekamilika. Maandalizi ya vyeti vya kuzindua miradi inaendelea.
    3
    Kidugala
    Masage
    Ufugaji wa mbuzi,kuku na nyuki
    22,321,428.56
    Mradi umekamilika. Maandalizi ya vyeti vya kuzindua miradi inaendelea.
    4
    Wanging’ombe
    Mayale
    Ufugaji wa kuku na mbuzi
    22,321,428.56
    Mradi umekamilika. Maandalizi ya vyeti vya kuzindua miradi inaendelea.
    5
    Kijombe
    Lyamluki
    Ufugaji Kuku,mbuzi na nyuki
    22,321,428.56
    Mradi umekamilika. Maandalizi ya vyeti vya kuzindua miradi inaendelea.
    6
    Saja
    Igenge
    Nyumba ya walimu Sekondari
    66,389,360.71
    Ujenzi umekamilika. Maandalizi ya vyeti vya kuzindua miradi inaendelea.
    7
    Usuka
    Usuka
    Nyumba ya walimu Sekondari
    66,389,360.71
    Ujenzi umekamilika. Maandalizi ya vyeti vya kuzindua miradi inaendelea.

    Kadhalika  kupitia mpango wa TASAF III, miradi mbalimbali ya kukuza kipato,uboreshaji miundombinu ya elimu na afya na ajira za muda(walengwa) imeendelea kutekelezwa ikifadhiliwa na OPEC III.

    3.2 MIRADI YA KUONGEZA KIPATO CHA KAYA MASIKINI

     

     

    MUDA

    WALENGWA WALIOKUSUDIWA

    WALENGWA WALIOLIPWA

    KIASI KILICHOLIPWA

    07/08/2015

    4,998

    4,924

    158,584,000

    09/10/2015

    4,988

    4,971

    145,976,000

    11/12/2015

    4,973

    4,967

    145,788,000

    01/02/2016

    4,998

    4,947

    145,456,000

    03/04/2016

    4,937

    4,920

    142,988,000

    05/06/2016

    4,937

    4,920

    142,988,000

    07/08/2016

    4,937

    4,893

    142,444,000

    09/10/2016

    4,907

    4,876

    141,900,000

    11/12/2016

    4,880

    4,872

    142,632,000

    01/02/2017

    4,926

    4,881

    133,414,000

    03/04/2017

    4,878

    4,843

    131,028,000

    05/06/2017

    4,827

    4,797

    132,412,000

    07/08/2017

    4,894

    4,784

    134,782,000

    JUMLA KUU

    1,840,392,000

    Hali ya utoaji fedha za Mpango wa kunusuru kaya Masikini Wilayani Wanging’ombe ni kama ifuatavyo:

    Katika Wilaya ya Wanging’ombe mpango huu ulianza  Mwaka 2015 kwa kufanya utambuzi na uandikishaji wa Kaya maskini ambapo  malipo ya kwanza kwa kaya stahiki yalianza rasmi Mwezi Julai,2015.

    Mpango huu ulizinduliwa Kitaifa katika Manispaa ya Dodoma na Mhe.Raisi Mstaafu Dkt. J.M.Kikwete mnamo Mwezi Agosti,Mwaka 2012.

    3.1 Mpango wa kunusuru kaya masikini unalenga kuhawilisha fedha kwa Kaya maskini ili kujikwamua kiuchumi na kuimarisha elimu na afya bora kwa watoto ikilenga kuboresha miundombinu ya elimu,maji na afya.

     3.0 MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI (TASAF III)

    Mikopo hii hurudishwa ndani ya muda wa  miezi 12 (mwaka mmoja) ambayo imegawanyika kwa robo 4 kila robo mkopaji anapaswa kurudisha kiasi cha fedha kinachotakiwa kurudishwa kwa robo husika.

    Mikopo hii hutozwa  riba ya 10% ambazo hurudishwa Halmashauri kwa ajili ya ufuatilijai mikopo na 2% hutozwa kwa ajili ya kuviwezesha  vyama vya ushirika(SACCOs) na kufanya 12%.

    Mikopo inayotolewa na Halmashauri ni lazima ipitie kwenye vyama vya ushirika (SACCOS) vilivyo karibu na  kijiji kinapotoka kikundi husika, hii huwezesha urahisi wa  ufuatiliaji wa vikundi na urejeshaji wa mikopo kwani mikopo hii ni`revolving Fund’ ni lazima waliokopeshwa warudishe ili vikundi vingine vinufaike  na mikopo hii.

    2.3 UTARATIBU WA UREJESHAJI

    Watalaam wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wakitoa mafunzo ya ujasiriamali kwa Wanavikundi vya Wanawake cha Amani Women Group na Tuinuane Ujindile- Kata ya Uhambule Januari,2017

     

    Uhamasishaji Vikundi vya Wanawake na maonyesho ya  shughuli za uzalishaji mali za Vikundi siku ya Wanawake Duniani 8 Machi,2017 Kijiji cha Igwachanya.

    Hali ya utoaji wa mikopo kwa vikundi inakabiliwa na uchache wa fedha hivyo mikopo inayolewa ni kidogo na kwa vikundi vichache kwa sababu Halmashauri inakabiliwa na majukumu ya lazima ya uendeshaji kutokana na mapato ya ndani kutumika kwa gharama za uendeshaji wa Halmashauri ambayo pia ni mpya na maelekezo ya lazima ikiwemo upelekaji 60% ya mapato ya ndani ya Halamashauri  kwa ajili ya shughuli za Maendeleo ngazi ya jamii.

     

    Vikundi cha Wanawake TUINUANE-Uhambule na Amani  Group–Ujindile Kata ya Uhambule wakipatiwa mafunzo ya uongozi,ujasiriamali  na taratibu za mikopo Januari, 2016.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE 31 JULAI 2024 July 31, 2024
  • KUITWA KWENYE USAIL September 27, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA UMILIKISHWAJI ARDHI February 13, 2021
  • Itizame yote

Habari mpya

  • TUZO ZATOLEWA KWA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025, NGAZI YA WILAYA - WANGING'OMBE.

    May 16, 2025
  • VIJIJI 10 VYA WANGING'OMBE KUNUFAIKA NA HATI ZA KIMILA 3,010

    May 13, 2025
  • BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI ROBO YA PILI YA MWAKA 2024/2025

    January 29, 2025
  • HERI YA SIKU YA KUZALIWA, MKURUGENZI MTENDAJI, DKT. PETER MAIGA NYANJA

    January 28, 2025
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.