• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

DC AAHIDI MATENGENEZO YA BARABARA ZA IVIGO – WANGING’OMBE

Tarehe iliyowekwa: October 2nd, 2025

Na. Nickson Kombe,


MKUU wa wilaya ya Wanging’ombe, Mhe. Zakaria Mwansasu aahidi matengenezo ya Barabara mbili tofauti zenye jumla ya kilomita 17.47 kiwango cha changarawe za Kijiji cha Ivigo kata ya Igosi wilayani wanging’ombe.


Akiongea na wananchi wa Kijiji cha Ivigo, Jumanne 30 Septemba 2025, katika mkutano wa kikazi wa kutembelea vijiji 108 wilayani humo, Mhe. Mwansasu ametoa fursa ya kusikiliza changamoto za wananchi kijijini hapo na moja ya changamoto hizo ni ubovu wa Barabara za Idunda-Ivigo-Igosi (Kilomita 9.4) na Barabara ya Ivigo-Igodivaha (Kilomita 8.07). Barabara hizo ni msingi wa maendeleo ya kijiji cha Ivigo kwa sababu hutumika kusafirishia mazao ya mbalimbali kama parachichi, viazi, ngano na mahindi.


Mhe. Mwansasu aahidi matengenezo ya Barabara hizo ili kuendeleza ustawi na maendeleo ya kijiji hiko na kuwataka wananchi hao kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kama kilimo ambapo Serikali itaendelea kushughulikia changamoto ya pembejeo za kilimo haswa bei za mbolea za mazao.


Akitolea ufafanuzi wa hatua za matengenezo ya Barabara hizo, Kaimu Meneja wilaya ya Wanging’ombe-TARURA, Mhandisi Anesporo Mwijuka amesema tayari Serikali imetenga kiasi cha milioni 138 kutengeneza Barabara ya Idunda-Ivigo-Igosi yenye kilomita 9.4 na kiasi cha milioni 134.2 kimetengwa kutengeneza Barabara ya Ivigo-Igodivaha yenye kilomita 8.07. Hatua iliyopo kwa sasa tayari Mkandarasi amepatikana taratibu za matengenezo zitaendelea muda mfupi ujao.


Aidha wananchi wa Kijiji cha ivigo wakiwakilishwa na Mwenyekiti wa Kijiji wamesema ubovu wa Barabara hizo unapelekea uuzwaji wa mazao kwa bei ndogo ukilinganisha na maeneo mengine hivyo wamesisitiza ukamilishaji wa matengenezo ya Barabara hizo kwa haraka zaidi ili kuondokana na bei ndogo za mazao yao.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI JIMBO LA WANGING'OMBE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025.. October 15, 2025
  • Itizame yote

Habari mpya

  • MCHUNGAJI AJITOLEA UKAMILISHAJI WA MADARASA MAWILI, S/M LUGODA

    October 07, 2025
  • HERI YA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA 2025.

    October 07, 2025
  • KAMATI YA USALAMA WILAYA YARIDHISHWA NA MIRADI SEKTA YA AFYA NA ELIMU - WANGING'OMBE.

    October 06, 2025
  • DC AAHIDI MATENGENEZO YA BARABARA ZA IVIGO – WANGING’OMBE

    October 02, 2025
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.