• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE

28 August 2017

HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING’OMBE

Barua zote ziandikwe kwa Mkurugenzi Mtendaji (W)

S.L.P 64,

NJOMBE

Unapojibu tafadhali taja;-

Kumb. Na. WDC/F.20/123 25.08.2017

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI.

1. UTANGULIZI.

Halmashauri ya Wilaya Wanging’ombe ni moja kati ya Halmashauri sita zilizopo kwenye Mkoa wa Njombe. Makao Makuu yake yapo katika Kata ya Igwachanya, Kijiji cha Igwachanya. Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe inakua kwa kasi kiuchumi na hii ni kutokana na kuboreka kwa shughuli za kiuchumi, mawasiliano na muingiliano wa watu. Sehemu kubwa ya uchumi inategemea kilimo cha mazao ya biashara kama vile Mahindi, Maharage, Miti, Alizeti, Viazi n.k.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe anawatangazia Wananchi wote Raia wa Tanzania wenye sifa kuomba kujaza nafasi zifuatazo.

2. MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III – TGS B (NAFASI 52).

2.1. Sifa za Muombaji;

Awe na Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV) au Sita (Form VI) aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani za Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya Sanaa kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma au Chuo chochote kinachotambulika na Serikali.

2.2. MSHAHARA.

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani Mshahara wa TGS B

2.3. KAZI NA MAJUKUMU

i. Afisa Masuuli na Mtendaji Mkuu wa Serikali za Kijiji,

ii. Kusimamia Ulinzi na Utawala Bora wa Raia na mali zao, kuwa mlinzi wa amani na msimamizi wa utawala bora katika Kijiji,

iii. Kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa mipango ya Maendeleo ya Kijiji,

iv. Katibu wa Mikutano na Kamati zote za Halmashauri ya Kijiji,

v. Kutafsiri na kusimamia Sera na Taratibu,

vi. Kuandaa taarifa za utekelezaji na kazi katika eneo lake na kuhamasisha uchumi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa umasikini na kuongeza uzalishaji mali,

vii. Kiongozi na mkuu wa Idara na Vitengo vya Kitaalam katika Kijiji,

viii. Kusimamia, kukusanya na kuhifadhi kumbukumbu na nyaraka za kijiji,

ix. Kujibu na kuandaa taarifa za utekelezaji wa kazi katika eneo lake na kuziwasilisha kwenye Halmashauri ya Kijiji na baadaye kwenye Mkutano Mkuu wa Kijiji na Kamati ya Maendeleo ya Kata,

x. Kupokea, kusikiliza na kutatua migogoro ya wananchi,

xi. Kusimamia utungaji na utekelezaji wa Sheria ndogo za Kijiji,

xii. Kusimamia ukusanyaji wa mapato katika kijiji,

xiii. Atawajibika kwa Mtendaji wa Kata na Mkurugenzi Mtendaji.

xiv. Kuandaa na kutunza rejesta ya wakazi wote Kijiji

3.0 DEREVA DARAJA LA II – TGOS A (NAFASI 2).

3.1 Sifa za Muombaji;

i. Awe mwenye cheti cha kidato cha Nne (Form IV) na leseni ya daraja E au C1 ya uendeshaji Magari ambaye amefanya kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja bila kusababisha ajali.

ii. Awe amehudhuria mafunzo ya msingi ya uendeshaji magari (Basic Driving Course) yanayotolewa na Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

iii. Waombaji wenye cheti cha majaribio ya Ufundi Daraja la II watafikiriwa kwanza.

3.2 MSHAHARA.

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani Mshahara wa TGOS A

3.3. Kazi na Majukumu;

i. Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari,

ii. Kuwapeleka watumishi maeneo mbali mbali kwenye safari za kikazi,

iii. Kufanya matengenezo madogomadogo ya gari,

iv. Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali,

v. Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari,

vi. Kufanya usafi wa gari,

vii. Kufanya kazi zingine kadri atakavyoelekezwa na msimamizi wako.

4.0 MASHARTI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.

i. Waombaji wote wawe Raia wa Tanzania na wenye Umri usiozidi miaka 45,

ii. Waombaji wote waambatanishe cheti cha kuzaliwa,

iii. Waombaji waambatanishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V.) yenye anuani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika,

iv. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya kidato cha nne na cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.

v. Testimonials, “provisional results”, “statement of results”, hati ya matokeo ya kidato cha nne na sita HAVITAKUBALIWA.

vi. Waombaji waambatishe picha moja ya “Passport size” ya hivi karibuni,

vii. Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 08 Septemba, 2017.

Maombi yote yatumwe kwa:-

Mkurugenzi Mtendaji (W),

Halmashauri ya Wilaya Wanging’ombe,

S.L.P. 64,

NJOMBE.

Imetolewa na:

MKURUGENZI MTENDAJI

HALMASHAURI YA WILAYA WANGING’OMBE

Matangazo

  • TANGAZO LA UMILIKISHWAJI ARDHI February 13, 2021
  • Badili Tahasusi kwa Wanafunzi Kidato cha Tano Tarajali na Vyuo vya Kati April 01, 2021
  • SIS MOBILE APPLICATION April 01, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA LEO 09 MEI,2021 May 09, 2021
  • Itizame yote

Habari mpya

  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA VITUO VYA AFYA VITATU (3) - 1,869,307,194 /=

    May 27, 2025
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA WA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, HOSPITALI YA WILAYA YA WANGING'OMBE

    May 20, 2025
  • TUZO ZATOLEWA KWA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025, NGAZI YA WILAYA - WANGING'OMBE.

    May 16, 2025
  • VIJIJI 10 VYA WANGING'OMBE KUNUFAIKA NA HATI ZA KIMILA 3,010

    May 13, 2025
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.