Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Wangingombe akiwa ziarani amekagua ujenzi wa madarasa,mabweni vyoo vinavyojengwa katika shule za Sekondari ikiwemo Shule ya Sekondari Mount Kipengere, Wanging'ombe,na Wanike Mkuu wa Mkoa amepongeza kwa kazi nzuri zilizofanywa na zinazoendelea kufanywa amesisitiza kutumia fedha za Serikali vizuri ili thamani ya fedha ioneekane katika miradi hiyo,pia alishauri kasoro mbalimbali alizoziona zirekebishwe mapema.Mkuu wa Mkoa alipata fursa ya kutembelea eneo ambapo itajengwa Hospitali ya Wilaya lililopo katika kijiji cha Ihanja amesisitiza kuwa eneo hilo ni zuri na mtu yeyote asiingilie eneo hilo,akiwa Wilaya ni huku alitembelea Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Palangawanu Mkuu wa Mkoa baada ya kupata fursa ya kutembelea mradi huo aliongea na wananchi na kutoa Maelekezo ya Serikali ambapo alimuagiza Mkurugenzi Mtendaji kusimamisha Shughuli za ujenzi zinazoendelea na kusema fedha zinazotumika katika ujenzi huo hazikulengwa kufanya kazi katika zahanati ya Palangawanu badala yake zilitakiwa kuboresha na kujenga majengo katika kituo cha Afya Wanging'ombe aliagiza fedha zote zilizobaki Tsh 300,000,000/= ziende Kituo cha afya Wanging'ombe na shughuli za ujenzi zianze mara moja huku akiahidi kuwachukulia hatua viongozi wate waliohusika na udanganyifu huo.
Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.