Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe amewaagiza wananchi wa Wilaya ya Wangingombe kuhakikisha wanafanya usafi katika maeneo yao ili kuhakikisha mazingira yanakuwa masafi na hivyo kuondokana na magonjwa yanayotokana na Uchafu mfano Kipindupindu,Mkuu wa Wilaya Kombred Brother Ally Kasinge ametoa maagizo hayo alipokuwa katika Kijiji cha Igwachanya yalipo Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya wakati akifanya ukaguzi wa usafi siku ya Jumamosi ya mwisho ya mwezi Septemba ameagiza kila ngazi kufuatilia usafi wa mazingiza katika kijiji cha igwachanya ambapo Mtendaji wa kata,Afisa Tarafa na Mkurugenzi Mtendaji na Wakuuu wake wa Idara wahakikishe usafi unafanyika ili kufikia Jumamosi ya Mwisho ya mwezi Oktoba maeneo yote yawe masafi .
Amon Chalamila
Wangingombe
Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.