Chanzo Ikulu
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu : +255-22-2114512, 2116898
Email : press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi : 255-22-2113425
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 07 Oktoba, 2017 amefanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri kwa kuongeza idadi ya Wizara, kuteua Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya na kuwahamisha Wizara baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri.
Katika mabadiliko hayo Mhe. Rais Magufuli ameongeza idadi ya Wizara na Mawaziri wake kutoka 19 hadi 21, na Naibu Mawaziri kutoka 16 hadi 21.
Iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini imegawanywa na kutakuwa na Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini, na iliyokuwa Wizara Kilimo, Mifugo na Uvuvi imegawanywa na kutakuwa na Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
Mhe. Rais Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ametangaza mabadiliko hayo Ikulu Jijini Dar es Salaam na lifuatalo ni Baraza la Mawaziri baada ya kufanyiwa mabadiliko.
I. Waziri – George Huruma Mkuchika
I. Waziri - Selemani Said Jafo
II. Naibu Waziri - Joseph Sinkamba Kandege
III. Naibu Wazri - George Joseph Kakunda
I. Waziri - January Yusuf Makamba
II. Naibu Waziri - Kangi Alphaxard Lugola
I. Waziri - Jenista Joackim Mhagama
II. Naibu Waziri - Anthony Peter Mavunde (Kazi, Vijana na Ajira)
III. Naibu Waziri - Stella Alex Ikupa (Walemavu)
I. Waziri - Dkt. Charles John Tizeba
II. Naibu Waziri - Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa
I. Waziri - Luhaga Joelson Mpina
II. Naibu Waziri - Abdallah Hamis Ulega
I. Waziri - Prof. Makame Mbarawa Mnyaa
II. Naibu Waziri - Mhandisi Atashasta Justus Nditiye
III. Naibu Waziri - Elias John Kwandikwa
I. Waziri - Dkt. Philip Isdor Mpango
II. Naibu Waziri - Dkt. Ashatu Kijaji
I. Waziri - Dkt. Medard Matogoro Kalemani
II. Naibu Waziri - Subira Hamis Mgalu
10. Wizara ya Madini.
I. Waziri - Angellah Kairuki
II. Naibu Waziri - Stanslaus Haroon Nyongo
I. Waziri - Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko
Kabudi.
12. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
I. Waziri - Dkt. Augustine Philip Mahiga
II. Naibu Waziri - Dkt. Susan Alphonce Kolimba
13. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga (JKT).
I. Waziri - Dkt. Hussein Ali Mwinyi
14. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
I. Waziri - Mwigulu Lameck Nchemba
II. Naibu Waziri - Mhandisi Hamad Yusuf Masauni
15. Wizara ya Maliasili na Utalii.
I. Waziri - Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla
II. Naibu Waziri - Josephat Ngailonga Hasunga
16. Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
I. Waziri - William Vangimembe Lukuvi
II. Naibu Waziri - Angelina Sylivester Mabula
17. Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
I. Waziri - Charles Paul Mwijage
II. Naibu Waziri - Mhandisi Stella Martin Manyanya
18. Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.
I. Waziri - Prof. Joyce Lazaro Ndalichako
II. Naibu Waziri - William Tate Ole Nasha
19. Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
I. Waziri - Ummy Ally Mwalimu
II. Naibu Waziri - Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile
20. Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
I. Waziri - Dkt. Harrison George Mwakyembe
II. Naibu Waziri - Juliana Daniel Shonza
21. Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
I. Waziri - Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe
II. Naibu Waziri - Jumaa Hamidu Aweso
Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Stephen Kagaigai kuwa Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kabla ya Uteuzi huo, Bw. Stephen Kagaigai alikuwa Kaimu Karani wa Baraza la Mawaziri.
Bw. Stephen Kagaigai anachukua nafasi ya Dkt. Thomas D. Kashilila ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Wateule wote wataapisha Jumatatu tarehe 09 Oktoba, 2017 saa 3:30 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
07 Oktoba, 2017
Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.