Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2017 zimezinduliwa rasmi katika uwanja wa Kumbukumbu Mjini Mpanda mkoani Katavi na unatarajiwa kuzunguka katika mikoa yote 31, ukipita kwenye Halmashauri 195 kwa muda wa siku 195.Kiongozi wa mbio hizo kwa mwaka huu ni Amour Amad Amour kutoka mkoa wa Kaskazini Unguja visiwani Zanzibar.
Kiongozi huyo atasaidiana na wenzake watano katika kukimbiza mwenge huo ambao ni pamoja na Bahati Mwaniguta Lugodisha (Geita), Bi Fatima Yunus Hassan (Kusini Pemba), Fredrick Joseph (Singida), Salome Obadia Mwakitalima (Katavi) na Shukran Islam Msumi (Mjini Magharibi).
Kauli mbiu ya mbio hizo kwa mwaka huu inasema "SHIRIKI KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YA NCHI YETU'
Mwenge huo wa Uhuru utakimbizwa Wilaya Wanging’ombe tarehe 30/04/2017 ambapo utakimbizwa takribani umbali wa kilomita 119.4 na kuzindua miradi saba.Ratiba yam bio hizo za Mwenge ni
Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.