• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA LISHE KWA VIJANA BALEHE - WANGING'OMBE

Tarehe iliyowekwa: October 28th, 2023

Na. Nickson Kombe,

Kuelekea kilele cha maadhimisho siku ya Afya na Lishe kwa Vijana Balehe, kitaifa yanayotarajiwa kufanyika Mkuranga, Mkoani Pwani. Wilaya ya Wanging'ombe imeadhimisha katika Kata ya Igwachanya, tarafa ya Mdandu ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni "Lishe Bora kwa Vijana balehe, Chachu ya Mafanikio Yao".

Akihotubia katika hafla fupi, Afisa Tarafa ya Mdandu, Bw. Emmanuel Kingu amewaasa wazazi kuzingatia lishe bora yenye virutubisho vyote ili kuboresha afya ya mwili na akili kwa watoto na familia kwa ujumla. Amenukuliwa akisema "Wilaya yetu imekua na matokeo mabaya baada ya tafiti za lishe, ijapokuwa tunalima na tunauza mazao mengi sana..., hivyo elimu ya lishe katika ngazi ya kaya iboreshwe zaidi ili kuhakikisha tunabadilisha utamaduni wa chakula kwa kuzingatia lishe bora..." ameyasema haya akiwa amealikwa kuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo.


Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya, Bw. David Hunja amesema ukosefu wa lishe bora kwa watoto na vijana umekuwa na athari ambazo hupelekea udhaifu  wa mwili na akili, kupungua kwa kinga na kukaribisha magonjwa ya moyo, shinikizo la juu la damu, saratani, kisukari, magonjwa ya figo n.k. Hivyo vijana wanapaswa kuzingatia lishe bora ili kukomboa taifa la baadae.

Utamaduni wa kuzingatia lishe bora unaendelea kuenezwa kwa vitendo, namna bora ya kufanya shughuli za kilimo bila kutumia viwatilifu vya kiwandani, ufugaji wa kuku na wanyama wengineo, unywaji wa maji mengi, kupunguza na kuacha matumizi ya vileo, dawa za kulevya, kupunguza ulaji wa vyakula vyenye mafuta, sukari na chumvi kwa wingi n.k. Jitahada zote hizo zimeendelea kufanywa kwa kuzingatia jamii inapata elimu ya lishe bora amesema hayo Afisa Lishe Wilaya, Bi. Zenobia Aloyce.


Aidha wazazi waaswa kuacha unyanyasaji kwa watoto, kutelekeza familia na kutozingatia ustawi wa familia, kukwepa majukumu yao ya msingi ambapo imeelezwa kuwa ndizo sababu zinazopelekea lishe duni kwenye familia.

Kwa upande wa Wananchi waliohudhuria hafla hiyo wameshukuru kwa kupata uelewa ya kuwa "Ni kheri kunywa lita moja ya maziwa kuliko vilevi..." ameyasema hayo Mwenyekiti wa Igwachanya.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE 31 JULAI 2024 July 31, 2024
  • KUITWA KWENYE USAIL September 27, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA UMILIKISHWAJI ARDHI February 13, 2021
  • Itizame yote

Habari mpya

  • TUZO ZATOLEWA KWA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025, NGAZI YA WILAYA - WANGING'OMBE.

    May 16, 2025
  • VIJIJI 10 VYA WANGING'OMBE KUNUFAIKA NA HATI ZA KIMILA 3,010

    May 13, 2025
  • BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI ROBO YA PILI YA MWAKA 2024/2025

    January 29, 2025
  • HERI YA SIKU YA KUZALIWA, MKURUGENZI MTENDAJI, DKT. PETER MAIGA NYANJA

    January 28, 2025
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.