• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

KAMATI YA SIASA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Tarehe iliyowekwa: August 27th, 2024

Na Mwandishi  Amon Chalamila

Mwenyekiti wa kamati ya siasa Wilaya ya Wanging’ombe Ndg Frank Chaula amelipongeza baraza la madiwani na wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya,ameyasema hayo Tarehe 26 -8-2024 wakati wa ziara ya ukaguzi wa Miradi iliyofanywa na kamati ya siasa ya Wilaya ya Wangingombe,Kamati ya siasa ilifanya ukaguzi wa miradi ya Afya katika Kata ya Ilembula ambapo mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya wenye thamani ya Tsh 500,000,000/-unatekelezwa,Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya iliyopo Kijiji cha Ihanja ambapo kamati ilikagua ujenzi wa jengo la upasuaji wanaume,Wodi la Wanaume na Jengo la kuhifadhia maiti pia kamati ilikagua mradi wa Ujenzi wa Zahanati ya Ng’anda,aidha katika ziara hiyo Pamoja na pongezi Kamati iliiagiza Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya Bi Claudia Kitta kuhakikisha maboma yote yanatengewa fedha na kumalizia kwa sababu wananchi wameshatekeleza kwa kiasi kikubwa, maboma yaliyoelekezwa kumaliziwa ni Jengo la Wagonjwa wa nje Kituo cha Afya Ilembula na Jengo la nyumba ya Watumishi Zahanati ya Ng’anda.” Wananchi wamefanya kazi kubwa kujenga maboma haya sasa si vema nguvu za wananchi zikapotea bure naagiza serikali kupitia Mkuu wa Wilaya kuielekeza Halmashauri kutenga fedha na kumalizia maboma haya ili wananchi wasione kama serikali yao imewatupa na kushindwa kuwaunga mkono katika jitihada zao za kujiletea maendeleo pia hili ni agizo la Mhe Waziri Mkuu hivyo mnapaswa kutekeleza mara moja” alisema Mhe Mwenyekiti waCCM Wilaya.Aidha Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya Bi Claudia Kitta alikiri kupokea maelekezo hayo ya Chama na Kuahidi kulifanyia kazi kwa haraka.Katika Ziara hiyo Pia Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Bi Agnetha Mpangile alishiriki huku akiahidi kuyafanyia kazi maelekezo ya Chama kwa Kuwasilisha katika Vikao vya Halmashauri na kufanyia maaamuzi.Katika Ziara hiyo Kamati ya Siasa walitembelea pia Soko la Igula ambapo wakala wa Chakula NFRA wananunua mahindi kutoka maeneo mbalimbali ya Wilaya, amabapo baada ya kufika eneo la soko la Igula kamati iliweza kukutana na wakulima wanaopeleka mazao yao na kuwaelekeza Wawakilishi wa NFRA kuhakikisha wanaongeza kasi ya upimaji mahindi na kuondoa foleni kubwa iliyopo “Tumepata taarifa kuwa kuna viashiria vya rushwa katika kununua mahindi ambapo wakulima hawapewi kipaumbele na badala yake mnawapa kipaumbele wafanyabiashara  sasa tunaomba mbadilike ikiwa nipamoja na kuongeza mizani na vitendea kazi vingine” alisema Mhe Mwenyekiti wa CCM  Wilaya.Aidha Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri Bi Agnetha Mpangile aliwasisitiza wananchi kuzingatia sheria kanuni na taratibu za Halmashauri kwa kuhakikisha wanalipa mapato ya Halmashauri.Aidha Mkuu wa Wilaya amesisitiza Wakulima kuhakikisha wanakuwa na barua inayowatambulisha kuwa ni wakulima kutoka katika vijiji wanakulima pale wanaposafirisha mazao yao vinginevyo wanapaswa kulipa ushuru wa Halmashauri ambao ndio unasaidia kutekeleza miradi ya maendeleo mbalimbali katika Wilaya” Hapa nisistize Sheria za Halmashauri zinakutaka kulipa ushuru pale unapokuwa umefanya biashara hivyo kama wewe ni Mkulima na unasafirisha mazao yako kupeleka NFRA hakikisha unapewa barua ya utambulisho kuwa ni mkulima na sio mfanyabiashara kwa sababu ni vigumu kubaini mkulima ni yupi na Mfanyabiashara ni yupi vinginevyo kama huna Barua ya utambulisho utapaswa kulipa Ushuru” alisema Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya.Aidha Kamati imepongeza na kuwaomba wananchi waiamini serikali yao ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe Daktari Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa kwa kuendelea kufanya kazi kwa bididi ili kuliletea Taifa Maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE 31 JULAI 2024 July 31, 2024
  • KUITWA KWENYE USAIL September 27, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA UMILIKISHWAJI ARDHI February 13, 2021
  • Itizame yote

Habari mpya

  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA VITUO VYA AFYA VITATU (3) - 1,869,307,194 /=

    May 27, 2025
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA WA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, HOSPITALI YA WILAYA YA WANGING'OMBE

    May 20, 2025
  • TUZO ZATOLEWA KWA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025, NGAZI YA WILAYA - WANGING'OMBE.

    May 16, 2025
  • VIJIJI 10 VYA WANGING'OMBE KUNUFAIKA NA HATI ZA KIMILA 3,010

    May 13, 2025
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.