DC WANGING'OMBE AFUNGA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA - UHAMBULE
Tarehe iliyowekwa: November 14th, 2023
Na Mwandishi Wetu,
Nickson Kombe,
Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe, Mheshimiwa Claudia Kitta amefunga mafunzo ya awali ya Jeshi la Akiba yaliyofanyika katika Kata ya Uhambule wilayani Wanging'ombe.
Mkuu wa Wilaya amesema Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuenzi mafunzo ya jeshi la akiba ili kuendeleza uzalendo, ukakamavu na ushupavu wa vijana wa kitanzania katika kulinda amani na usalama uliopo nchini.
Katika Mafunzo hayo, jumla ya Askari wapya 90 wamefanikiwa kuhitimu ambapo wanaume 80 na wanawake 10. Aidha, vijana waliohitimu mafunzo hayo wana fursa za kupata ajira katika sekta za umma na binafsi.
Hata hivyo ametumia fursa hiyo kuwapongeza wale wote waliofanikiwa kuhitimu mafunzo hayo, "Hongereni sana kwa wale mliofanikiwa kuhitimu mafunzo haya yaliyoanza tarehe 07 Julai 2023, kutokana na uzalendo mlionao mmeweza kuhitimisha mafunzo haya mkiwa 90 kwa idadi".