• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

BARAZA LA MADIWANI WANGING’OMBE LAPINGA MUENDELEZO WA MATUMIZI YA DAMPO LA ITENGELO KAMA ENEO RASMI LA KUTUPA TAKA ZA MJI WA MAKAMBAKO

Tarehe iliyowekwa: October 31st, 2023

Na Mwandishi Wetu,

Nickson Kombe,



Baraza la Madiwani, Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe wamepinga vikali kitendo cha matumizi sehemu ya eneo lililopo Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja, Wanging’ombe kama sehemu ya kutupa taka za mji wa Makambako.

Akiongea katika baraza la madiwani la mwezi Oktoba, Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Onesmo Lyandala amesema wameazimia kwa pamoja kupinga matumizi ya eneo hilo kama eneo rasmi la kutupa taka za mji wa Makambako, kutokana na uchunguzi uliofanywa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na kubaini ya kuwa kuna muingiliano mkubwa wa taka hizo na mifereji ya maji iliyopo karibu na sehemu hiyo.


Ardhi hiyo iliyopo Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja inayokadiriwa kuwa ekari 25, eneo hilo linamilikiwa na mtu binafsi. Kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa matumizi ya ardhi hiyo, ambapo Halmashauri ya Mji wa Makambako wameendelea kutumia eneo hilo kama dampo rasmi la kutupa taka za mji huo muda mrefu. Kipindi cha mgawanyo wa ardhi za Halmashauri 2010, eneo hilo lilikuwa ndani ya umiliki wa Halmashauri ya Njombe, baadae Mwaka 2012 likamilikishwa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe. Idhini ya muendelezo wa matumizi ya eneo hilo iliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mnamo wa Julai 2016, na baadae Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kutoa katazo la kimazingira mnamo wa Februari 2019 “Environmental Protection Order” kuzingatia sheria ya mazingira 2004 ambayo “imeweka bayana kila Halmashauri husika kutenga maeneo ya taka ndani ya mipaka yao…na sio vinginevyo” ili kuepusha migogoro na kuendelea kutunza mazingira kwa kufuata taratibu zote za uhifadhi wa mazingira bila athari.


Hata hivyo dampo hilo la Itengelo kijografia lipo karibu na chanzo cha maji kinachotiririsha maji kuelekea kitongoji cha Makonda. Kipindi cha mvua mifereji ya maji hupelekea muingiliano wa taka hizo na kuleta athari kwa watumiaji wa maji hayo.

Aidha Baraza la madiwani wamepinga hilo ili kuepusha athari za kimazingira zinazotokana na muendelezo wa kutupa taka katika dampo hilo.








Matangazo

  • TANGAZO LA UMILIKISHWAJI ARDHI February 13, 2021
  • Badili Tahasusi kwa Wanafunzi Kidato cha Tano Tarajali na Vyuo vya Kati April 01, 2021
  • SIS MOBILE APPLICATION April 01, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA LEO 09 MEI,2021 May 09, 2021
  • Itizame yote

Habari mpya

  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA VITUO VYA AFYA VITATU (3) - 1,869,307,194 /=

    May 27, 2025
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA WA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, HOSPITALI YA WILAYA YA WANGING'OMBE

    May 20, 2025
  • TUZO ZATOLEWA KWA WAKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025, NGAZI YA WILAYA - WANGING'OMBE.

    May 16, 2025
  • VIJIJI 10 VYA WANGING'OMBE KUNUFAIKA NA HATI ZA KIMILA 3,010

    May 13, 2025
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.