Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Mhe. Claudia Kitta Ameongoza jopo la Watumishi na Wananchi kufanya Usafi wa Mazingira katika Hospitali ya Wilaya IHANJA Kata ya Mdandu.
Ziara ya Usafi wa Mazingira kwa kauli Mbiu ya "Mazingira ni Afya" inaazimia katika Kuungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru Tarehe 9-12-2023
Kila mwananchi anawajibu wa kutunza Mazingira kuepuka milipuko ya magonjwa Kama, Malaria, Kipindupindu ,magonjwa ya kutapika na magonjwa ya tumbo.