ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA WANGING'OMBE KATIKA HOSPITALI YA WILAYA - IHANJA
Tarehe iliyowekwa: November 26th, 2023
Na. Mwandishi Wetu,
Rukia Omary,
Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Mhe. Claudia Kitta ameambatana na Wataalamu wa Wadau wa Afya kutoka Shirika lisilo la Kiserikali Helen Keller International - HKI, ambao wamewezesha programu maalumu ya Operesheni ya Mtoto jicho katika Hospitali ya Wilaya ya Ihanja. Katika Ziara hii Mkuu wa Wilaya ametembelea wodi mbalimbali za huduma za awali na walizolazwa wagonjwa wa Operesheni ya macho.
Mkuu wa Wilaya amefurahishwa na huduma hii ya macho inayotolewa na Shirika la Helen Keller International kwa Kuonesha uzalendo kwa Wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe kwakutambua mchango wa kuwafikishia huduma hii ya matibabu pia kutoa Shukrani kwa uongozi wa awamu ya sita wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua mchango wake wa Matibabu kwa Wananchi pia Wizara ya Afya na TAMISEMI kwa Kushirikiana na Shirika Hili kuleta huduma Vijijini.
Kwa upande wake Meneja Mradi wa Shirika lisilo la kiserikali na Mdau wa Afya Bw. Athman Tawakal amesema anashukuru sana kwa wananchi wengi kujitokeza na kupata matibabu kwa jitihada za wahudumu wa afya ngazi ya jamii walipita kaya kwa kaya kuwabaini wagonjwa na mpaka sasa matibabu yametolewa kwa wagonjwa 185 shirika hili limelenga kufanya matibabu zaidi ya wagonjwa 300 na tumeanza na kata chache katika wilaya hii yenye idadi ya vijiji 108 na kata 21 hivyo tunashukuru kwa ushirikiano tulioupata kutoka kwa jamii bado jamii inahitaji huduma hii, hivyo bado huduma hii ni endelevu na tunaendelea kuitoa kwa kushirikiana na timu ya madaktari na zoezi hili linahusisha wananchi wote bila gharama yoyote.
Aidha, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Dkt. Frank Chiduo ameshukuru Shirika hili kuwezesha huduma katika Wilaya hii na kujivunia kuwa Wilaya ya Kwanza kuzindua Matibabu haya hivyo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza na kupata huduma hii
Wananchi wanaipongeza serikali kwa kuwajali,kuwathamini na kutambua umuhimu wa wananchi wake hasa katika kushiriki katika shughuli za kijamii.