Na. Nickson Kombe,
WAZAZI na walezi wametakiwa kuwa msatari wa mbele katika kukemea vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa watoto ili kutokomeza/kupunguza vitendo hivyo viovu katika jamii na kuendelea kubaki salama.
Maoni hayo yamesemwa leo Februari 10, 2026 na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe, Wakili Joshua Sanga katika kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama dhidi ya Ukatili wa Wanawake na Watoto ambapo kikao hiko kimefanyika ukumbi wa Halmashauri, ikiwa lengo ni kufanya tathimini ya utekelezaji wa shughuli za Ustawi wa jamii, kikishirikisha viongozi wa dini, Afisa wa Dawati la Jinsia-Polisi, Hakimu wa Mahakama ya Wilaya, Maafisa Elimu wa Sekondari na Msingi, Afisa Uhamiaji, Askari Magereza na Taasisi isiyo ya kiserikali “UWODO”.
Wazazi wameshauriwa “kuwakagua na kuongea na watoto wao kirafiki zaidi ili kuweza kutambua changamoto mbalimbali hasa za vitendo vya ukatili zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi kabla ya kuleta madhara ikiwa pamoja na kutoa taarifa kwenye mamlaka husika hususani Jeshi la Polisi” ameyasema hayo Wakili Sanga.
Kwa upande wa maafisa Ustawi wa jamii wameshauriwa kuendelea kuwa shirikishi na kujiongeza kutumia mbinu mbadala ili watakaobainika Kutenda vitendo vya ukatili kwa Watoto/wanawake kufikishwa mbele ya mkono wa sheria na kuhukumiwa ili jamii ipate funzo. Hali ambayo itapelekea kuwa na jamii zenye maadili bora, afya njema na kupelekea kukua Uchumi wa kaya na nchi kwa ujumla, ameyasema hayo Kaimu Mganga Mkuu, Wanging’ombe, Dkt. Fransis Hoya.
Aidha Wasilisho la Afisa Ustawi wa Jamii, Bw. Barnabas Sichone ameweka bayana changamoto wanazokumbana nazo katika kazi zao ikiwemo kukosa Ushahidi au Mashahidi kutokutoa ushirikiano pindi wanapohitaji kuchukua hatua za kisheria dhidi ya watuhumiwa ambapo wameendelea kutoa elimu kwenye jamii na wanatumia kauli mbiu isemayo “KUANZIA SASA, NASIMAMA IMARA, SITANYAMAZA TOKOMEZA UKATILI”.










Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.