WANANCHI MSIMBAZI WANUFAIKA NA MRADI WA TASAF
Kaimu Mwenyekiti Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango Mhe Paulina Samata Mwinami , ametoa shukrani zake za dhati kwa TASAF kwa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa, vyenye jumla ya thamani ya Tsh 34,764,213.18/= Mhe alitoa pongezi hizo katika kijiji cha Msimbazi hivi karibuni wakati wa ukaguzi wa Miradi ya maendeleo inayotekelezwa.Katika ziara hiyo Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri aliongozana na wajumbe wa kamati hiyo.
Aidha wajumbe wa kamati walipongeza jitihada za wananchi kwa kuchangia nguvu kazi katika mradi huo,kwani TASAF walitoa jumla ya Tsh 65,014,285.53/= na kutumia kiasi cha Tsh 34,764,213.18/= hivyo kubakiwa na Tsh 30,250072.53/= zitakazofanya shughuli nyingine. “Nawaomba wananchi wenzangu tuendelee kuchangia nguvu kazi katika miradi hii inayoletwa na Serikali ili tuweze kummuunga Mkono Mhe Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano katika jitihada za kuleta maendeleo”.alisema
Katika ziara hiyo kamati ilikagua miradi mingine inayotekelezwa ndani ya Halmashauri miradi hiyo ikiwa ni
Aidha wajumbe waliwapongeza wataalam kwa kusimamia vema Miradi hiyo na kuwataka waendelee kusimamia miradi inayoendelea kutekelezwa, pia kushirikisha wataalamu katika maeneo husika miradi inakotekelezwa.
Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.