• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Wanging'ombe District Council
Wanging'ombe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Kilimo
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Mazingira
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Kitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha uongozi na Mipango
      • Kamati ya UKIMWI
      • Maadili
      • Uchumi,Afya na Elimu
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Gazeti la Serikali
    • Sheria ndogo za Halmashauri
    • Mpango mkakati wa Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

TIMU YA MAPATO YAPONGEZWA KUFIKIA ASILIMIA 71, LENGO LA UKUSANYAJI MAPATO 2025/26.

Tarehe iliyowekwa: February 6th, 2026

Na. Nickson Kombe,


MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe, Dkt. Peter Maiga Nyanja amewapongeza timu yote ya mapato kwa kufikia asilimia 71 ya lengo la ukusanyaji mapato mwaka wa fedha 2025/26 katika kikao kazi kilichofanyika Ukumbi wa Halmashauri.


Pongezi hizo zimetolewa leo tarehe 06 Februari 2026, wakati akizungumza na timu ya wakusanya mapato wa Halmashauri, Dkt. Nyanja amesema anatarajia ifikapo machi 2026, timu hiyo itakua imevuka malengo hivyo waendelee kufanya kazi kwa weledi na ubunifu zaidi ili kudhibiti mianya mbalimbali ya uchepushaji wa mapato ya Halmashauri.


“Pamoja na changamoto zilizopo, natumia fursa hii kuwapongeza kwa ukusanyaji mzuri wa mapato, nimejulishwa ya kuwa mwaka huu mnataka kuvuka lengo na kwa takwimu za wiki iliyopita mmefika asilimia 71 hivyo sina shaka naamini kufikia Machi 2026 mtafuka lengo, hii inaonesha ni namna gani mnafanya kazi kwa kujituma na kwa ushirikiano. Pongezi kwenu,” alisema Dkt. Nyanja.


Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe imepangiwa kukusanya Shilingi Bilioni 5.4 mapato halisi kwa mwaka wa fedha 2025/2026. hadi kufikia mwisho wa mwezi Mei 2026. Mpaka kufikia mwisho wa mwezi Januari 2026, Halmashauri imekusanya Shilingi Bilioni 3.8 sawa na Asilimia 71 ya lengo, ikiwa ni ongezeko la asilimia 2 ukifananisha na mwaka wa fedha uliopita 2024/25.


Hivyo timu ya wakusanya mapato wa Halmashauri ikiwakilishwa na Mwenyekiti wao, Bw. Frank Kassano ametumia fursa hiyo kutoa neno la shukrani kwa uongozi dhibiti wa Mkurugenzi Mtendaji, Dkt. Peter Maiga Nyanja kwa namna ambavyo amekuwa akiwajali katika maslahi yao, haki na kuwawezesha kufanya kazi katika mazingira rafiki zaidi. Hivyo timu hiyo imemzawadia Mkurugenzi Mtendaji, Dkt. Nyanja zawadi kede kede.


Aidha Mafanikio haya yanaiweka Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe katika ramani ya Halmashauri zinazotekeleza vyema maelekezo ya Serikali ya kuboresha ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuongeza uwezo wa kuwahudumia wananchi na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wakati.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI JIMBO LA WANGING'OMBE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025.. October 15, 2025
  • Itizame yote

Habari mpya

  • DKT. NINDI AAHIDI KUFANYA MKOA WA NJOMBE KUWA WA KIPEKEE ZAIDI.

    February 13, 2026
  • MITI 2,000 YAPANDWA KATIKA MJI WA IGWACHANYA-WANGING'OMBE.

    February 12, 2026
  • WAZAZI WAASWA KUWALINDA WATOTO DHIDI YA VITENDO VYA UKATILI - WANGING’OMBE.

    February 11, 2026
  • ELIMU YA BIMA YA AFYA KWA WOTE (NHIF) YATOLEWA KWA WADAU WA AFYA.

    February 06, 2026
  • Itizame yote

Video

MAKALA YA MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN WILAYA YA WANGING'OMBE
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Vivutio vya Utalii Wanging'ombe
  • Historia ya Halmashauri ya Wanging'ombe
  • Mfumo wa Mawasiliano ya ndani wa Serikali Government Mailing System (GMS)
  • Registration Of Allied Health Professionals
  • Mfumo wa maombi ya Ajira
  • baraza la taifa la elimu ya ufundi

Tovuti Mashuhuri

  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi kwa watumishi wanaopewa ruhusa na Katibu Mkuu Kiongozi
  • Mfumo wa Malalamiko na Pongezi
  • UTUMISHI
  • MFUMO WA SIS(SCHOOL INFORMATION SYSTEM)
  • TAMISEMI
  • BUNGE

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani

Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.