Wananchi Wilayani Wanging'ombe wameaswa kutumia fedha vizuri ili kuleta tija katika shughuli zao za kiuchumi, Wananchi hao wameaswa na Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Comrade Ally Kasinge tarehe 23/01/2019 katika ukumbi wa Halmashauri uliopo Igwachanya, wakati wa hafla ya ugawaji wa hundi kwa vikundi vya akina mama, vijana na Walemavu aidha jumla ya Tsh Milioni 94 zimegawiwa kwa vikundi 45 vyenye idadi wanawake 225 vijana 90 na walemavu15.”Ninayo furaha kubwa leo kushiriki katika uzinduzi wa utoaji wa mikopo isiyo na riba kwa vijana,wanawake na walemavu.utoaji wa mikopo hii unalenga kutekeleza ilani ya uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 sura ya tano ambayo ni uwezeshaji wananchi kiuchumi.Serikali inatambua kwamba kuwawezesha wananchi kiuchumi ni hatua ya msingi katika kujenga Taifa lililo imarika kiuchumi na lenye lengo la kuijtegemea” Alisema Mkuu wa Wilaya.
Aidha katika hafla hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe Mhe Emmanuel Mahwata aliwataka wanufaika wa fedha hizo kuzitumia vizuri ili ziweze kuongeza kipato na hivyo kutimiza lengo la Serikali la kukuza uchumi.Aliwakumbusha kuwa fedha hizo zinatokana na mapato ya Ndani ya Halmashauri ambapo yeye ndie msimamizi mkuu na kuwaomba kuwahimiza wananchi kuweza kulipa tozo mbalimbali za Halmashauri ili jambo hilo liwe endelevu kwani bila Kukusanya fedha hizo ambazo ni asilimia 10 ya makusanyo haziwezi kupatikana.Pia aliwasihi wanufaika wa makundi yote kurejesha kwa wakati fedha hizo kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.
Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.