Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Wangingombe imefanya ziara ya ukaguzi wa Miradi inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya, katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Kuiona Wanging’ombe na Kutoa fedha kwa ajili ya Utekelezaji wa miradi mbalimbali ili kuboresha huduma kwa Wananchi wake.”Napenda kumpongeza Mhe Rais wa Awamu ya sita kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuwaletea maendeleo Wananchi hadi kupelekea kupata fedha hizi zinazotekeleza miradi” alisema Mwenyekiti Ndg Stephano Pesambili Kinyangadzi wakati wa ukaguzi wa miradi siku ya jumanne katika Vijiji vya Ihanja panapojengwa Hospitali ya Wilaya ikiwa ni ujenzi wa wodi tatu za Wanawake,Watoto na Wanaume,Kijiji cha Mdandu panapojengwa Madarasa mawili na Ofisi,Makoga panapojengwa Kituo cha Afya na ukarabati wa jengo la Utawala katika Shule ya Sekondari Makoga,Samaria panapojengwa Zahanati ya Kijiji na Masage panapojengwa Madarasa mawili pamoja na Ofisi.Pia Mwenyekiti alitoa Pongezi kwa Mhe Mbunge wa Jimbo la Wanging'ombe na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tamisemi Ndg Festo John Dugange kwa kazi nzuri anayoifanya na kumwomba aendelee na moyo huo ambao ameanza nao kwani ameleta fedha nyingi kwa kipindi kifupi ambazo kila Kata imeguswa.
Zikisomwa Taarifa za utekelezaji wa miradi hiyo Jumla ya fedha takribani Millioni 800 zimetolewa na Serikali kutekeleza Miradi hiyo na hatua ya utekelezaji ikiwa katika hatua za umaliziaji.
Aidha katika ziara hiyo alikuwepo Mhe Mkuu wa Wilaya Ndg Lautery Kanoni ambae pia ni mjumbe wa Kamati ya Siasa pamoja na Wataalmu kutoka Halmashauri ambapo Mhe Mkuu wa Wilaya aliwapongeza wataalamu na Wananchi kwa kusimamia na kutekeleza miradi vizuri licha ya changamoto ndogondogo zilizopo alimhakikishia Mwenyekiti kuwa atasimamia vema shughuli hizi ili kuhakikisha Miradi inakamilika kwa wakati ikiwa yenye Kiwango kwa sababu yeye ndie msimamizi wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi.
Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.